Saturday, 28 December 2019

MKUTANO WA SOLVAY WA MWAKA 1927

ulivyowakutanisha watu wenye akili zaidi duniani kwa pamoja
Huu ulikuwa ni muendelezo wa mikutano iliyokuwa inawakutanisha wataalamu waliobobea kwenye taaluma za Fizikia na Kemia wakijadili masuala mbali mbali kuhusu taaluma hizo
Mkutano wa kwanza ulikuwa mwaka 1911 ulifanyika nchini ubelgiji huku mwenyekiti wao akiwa ni Hendrick Lorentz .....katika mkutano huo walijadili kuhusu Quantum Theory na classical physics
Mwaka 1927 ulifanyika mkutano wa tano wa kimataifa wa Solvay ...mkutani huu ukiwakutanisha wanafizikia wa dunia na walioacha historia ya sayansi kuwa hivi ilivyo
Kwenye mkutano huo walikuwa wanajadiliana kuhusu fomula mpya ilioundwa kuhusu nadharia ya quantum ...ambapo Albert Einstein na Niels Bohr ndio walikuwa waongeaji wakuu

Katika mkutano wa mwaka 1927 uliwakutanisha wanasayansi 29 na kati ya hao 17 walishinda tuzo ya noble akiwemo mwanamama Currie aliyeshinda tuzo ya Noble katika taaluma mbili tofauti ya kemia na fizikia
Majina yao kuanzia Nyuma na kuanzia kushoto kwenda kulia
Auguste Piccard, Émile Henriot, Paul Ehrenfest, Édouard Herzen, Théophile de Donder, Erwin Schrödinger, Jules-Émile Verschaffelt, Wolfgang Pauli, Werner Heisenberg, Ralph Howard Fowler, Léon Brillouin,
Peter Debye, Martin Knudsen, William Lawrence Bragg, Hendrik Anthony Kramers, Paul Dirac, Arthur Compton, Louis de Broglie, Max Born, Niels Bohr,
Irving Langmuir, Max Planck, Marie Skłodowska Curie, Hendrik Lorentz, Albert Einstein, Paul Langevin, Charles-Eugène Guye, Charles Thomson Rees Wilson, Owen Willans Richardson

No comments:

Post a Comment