Hotel hiyo iliyotengenezwa katika mji wa maka nchi saudia arabia imegharimu Dolar za kimarekan Bilion 3.5 .....itakuwa na vyumba 10,000 na migahawa 70 na maduka makubwa ya bidhaa mbalimbali
Mji wa Maka una uhakika wa kupokea zaidi ya Mahujaji Milion 2 kila mwaka kwa ajili ya kufanya hija katika mji huo mtukufu wa waislamu
Lakini pia Mji wa Maka kwa mwaka mmoja unapokea zaidi ya Wageni Milion 20 ambao wanakwenda kwa ajili ya kutembea tu
Hotel hiyo itakuwa na vyumba vya kifahari kwa ajili ya watu matajiri, lakini pia kitakuwa na eneo maalumu kwa ajili ya familia ya kifalme ya nchi hiyo
Hotel hiyo imechukua eneo lenye ukubwa wa meter square 1,400,000
Itakuwa majengo marefu 12
Kwa sasa rekodi ya hotel kubwa inashikiliwa na hotel ya Genting Highland ya nchini Malaysia....hotel hiyo ina vyumba 7,351 kwa mchanganuo ufuatao
Standard rooms 3164
Deluxe rooms 2922
Triple deluxe rooms 649
Superior deluxe rooms 480
World club rooms 136
Ukijumlisha vyumba vyote hivi ndio unapata vyumba 7351 vya hotel hii inayoshikilia rekodi ya dunia kwa sasa....hadi hapo Abraj Kudai itakapofunguliwa
No comments:
Post a Comment