Saturday, 28 December 2019

HOTEL KUBWA ZAIDI DUNIANI kufunguliwa 2020

Abraj Kudai ndio hotel itakayoshikilia rekodi ya ukubwa zaidi duniani pindi itakapoanza kutumika mwaka 2020

Hotel hiyo iliyotengenezwa katika mji wa maka nchi saudia arabia imegharimu Dolar za kimarekan Bilion 3.5 .....itakuwa na vyumba 10,000 na migahawa 70 na maduka makubwa ya bidhaa mbalimbali

Mji wa Maka una uhakika wa kupokea zaidi ya Mahujaji Milion 2 kila mwaka kwa ajili ya kufanya hija katika mji huo mtukufu wa waislamu

Lakini pia Mji wa Maka kwa mwaka mmoja unapokea zaidi ya Wageni Milion 20 ambao wanakwenda kwa ajili ya kutembea tu

Hotel hiyo itakuwa na vyumba vya kifahari kwa ajili ya watu matajiri, lakini pia kitakuwa na eneo maalumu kwa ajili ya familia ya kifalme ya nchi hiyo

Hotel hiyo imechukua eneo lenye ukubwa wa meter square 1,400,000

Itakuwa majengo marefu 12

Kwa sasa rekodi ya hotel kubwa inashikiliwa na hotel ya Genting Highland ya nchini Malaysia....hotel hiyo ina vyumba 7,351 kwa mchanganuo ufuatao

Standard rooms 3164

Deluxe rooms 2922

Triple deluxe rooms 649

Superior deluxe rooms 480

World club rooms 136

Ukijumlisha vyumba vyote hivi ndio unapata vyumba 7351 vya hotel hii inayoshikilia rekodi ya dunia kwa sasa....hadi hapo Abraj Kudai itakapofunguliwa

Image may contain: sky, cloud and outdoor

No comments:

Post a Comment